Filed under: HABARI

Mbunge wa Bumbuli na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Habari na Masoko ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambaye hivi karibuni pia ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa January Makamba(Pichani juu) hivi karibuni ameainisha adhma yake ya kuinua kiwango cha michezo nchini.
Azma hizo zimo katika katika mazungumzo yake na Padre Privatus Karugendo ambayo yamechapishwa katika kitabu ambacho gazeti hili imekipata nakala yake ambapo ameainisha azma ya kujenga vitua vya michezo vya kanda vyenye hadhi ya kiolimpiki.
Kwenye kitabu hicho, Makamba amejibu swali kwamba kitu gani kifanyike ili Watanzania waweze kujivunia wanamichezo wao. Makamba alisema, “Inafedhehesha sana kuona kwamba asilimia 79 ya Watanzania walikuwa hawajazaliwa mara ya mwisho tumeshiriki katika fainali za kombe la mataifa ya Afrika.
Mwaka huo huo wa 1980 ndio mara ya kwanza na ya mwisho tuliweza kushinda medali za Olimpiki. Rafiki yangu Mzee Suleiman Nyambui na Mzee wetu Filbert Bayi ndio walitutoa kimasomaso kipindi kile. Ni muhimu kurekebisha hili.”
Ni ukweli usiopingika kwamba Tanzania imekuwa kama kichwa cha mwendawazimu katika medani ya kimataifa huku tasnia ya michezo ikiendelea kugubikwa na migogoro isiyokwisha. Kutokana na migogoro hii, Tanzania inaendelea kupoteza matumaini ya kung’aa katika medani za kimataifa.
Katika mazungumzo hayo na Padre Karugendo, Makamba alinukuliwa akisema, “Lazima tutambue kwamba maendeleo ya michezo yanatokana na vitu muhimu vitatu. Kwanza, ni lazima kuwepo na vipaji, bahati nzuri nchi yetu ina vipaji vya kutosha katika aina zote za michezo. Pili, ni miundombinu na mfumo wa kubaini na kuviendeleza vipaji hivyo, hii bado ni changamoto . Tatu, ni utawala, uongozi, na uendeshaji wa tasnia ya michezo, hii pia ni changamoto. Hivi vitu vitatu ni lazima viwepo ili tuweze kupata mafanikio kwenye medani ya michezo.”
Kama mgombea wa kwanza kutangaza nia yake ya kugombea nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, Makamba anaungwa mkono na vijana wengi kutokana na kuendesha siasa zake kisasa, kibunifu na kuepuka malumbano ya jukwaani.
Katika mazungumzo hayo Makamba alielezea fikra zake alizonazo hasa hasa kwenye kuendeleza vipaji vya Watanzania ambapo alisema, “Ni lazima tuanzishe vituo vikubwa vya michezo au ‘sports academies’ kwenye kila kanda ya nchi yetu vyenye hadhi ya Kiolimpiki.”
Makamba aliongeza kwamba, “Kutakuwa na vituo sita vya aina hii katika nchi yetu ambavyo vitazungukwa na shule za msingi na sekondari za ‘boarding’. Vituo hivi vitakuwa na lengo la kukusanya wanafunzi wote kwenye kanda husika ambao wameonekana kuonyesha vipaji ambavyo vinapaswa kuendelezwa. Ukweli ni kwamba bila kuendeleza vipaji katika mazingira mazuri, basi tusahau kabisa kufanya vizuri kwenye michezo. Hili linaweza kufanywa kwa ushirikiano wa serikali na sekta binafsi”.
Mheshimiwa January Makamba anakuwa mgombea wa kwanza wa Urais kuweka bayana mipango yake ya Tanzania Mpya katika maandishi. Anaendelea kufunguka kwamba katika tasnia ya michezo ni muhimu sana kuwekeza katika watoto. Zaidi ya hapo, kila timu ya ligi kuu ni lazima iwe na akademi na TFF iendeshe ligi kuu ya timu za watoto.
“Tufikie wakati ambapo timu za taifa za miaka 10 ijayo ziwe zinaandaliwa kuanzia sasa, na serikali itenge bajeti kila mwaka kwa timu hizo ili kuziwezesha kukaa kambini, kufanya mechi za majaribio na kuziwezesha kushiriki kikamilifu katika mashindano ya kimataifa. Mimi sio muumini wa hizi kamati za zimamoto kusaidia timu ishinde ghafla ghafla wakati siku zote watu hawafanyi maandalizi ya muda mrefu” alimalizia Makamba.
Makamba pia aligusia kuhusu suala la ukata na ufinyu wa bajeti unaokabili tasnia za michezo. Siku zote tunaona timu za taifa za olimpiki au jumuiya ya madola kukosa fedha za kukaa kambini ambapo huchangia katika matokeo hafifu.
“Huko nyuma, taasisi na mashirika ya umma yalikuwa na timu za michezo zilizokuwa zinafanya vizuri na kutoa michango kwenye maendeleo ya michezo. Kwa mfano, Pamba ya Mwanza, Sigara, Reli ya Morogoro, ushiriki huu ulichangamsha sana michezo na ni lazima turudishe utamaduni huu,” alimalizia Makamba.
Mbunge wa Arumeru Magharibi Goodluck Ole Medeye akifafanua jambo katika kikao cha Baraza la madiwani kilichojadili bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Arusha mjini kwa mwaka 2015/2016 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 42.7 zimetengwa kusaidia upatikanaji wa huduma za maji,afya na elimu kama vipaumbele vikuu.Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha Fidelis Lumato,Mwenyekiti wa Halmashauri Saimon Saning`o na kaimu Mwenyekiti Anna Agatha Msuya.Kikao hicho kilifanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri.(Habari picha na Ferdinand Shayo wa Jamiiblog)
Mbunge wa Arumeru Magharibi Goodluck Ole Medeye akifafanua jambo katika kikao cha Baraza la madiwani kilichojadili bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Arusha mjini kwa mwaka 2015/2016 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 42.7 zimetengwa kusaidia upatikanaji wa huduma za maji,afya na elimu kama vipaumbele vikuu.Kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Mwenyekiti Anna Agatha Msuya. Kikao hicho kilifanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha Fidelis Lumato akielezea juu bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Arusha mjini kwa mwaka 2015/2016 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 42.7 zimetengwa kusaidia upatikanaji wa huduma za maji,afya na elimu kama vipaumbele vikuu.Katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri Saimon Saning`o na Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Mwenyekiti Anna Agatha Msuya. Kikao hicho kilifanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha vijijini ,Fidelis Lumato amesemakuwa wilaya yake imepanga bajeti ya kiasi cha shilingi bilioni 42 kwa mwaka wa fedha 2015 /2016 ambazo zitaelekezwa kwenye masuala ya maji,afya na elimu ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.
Fidelis Lumato aliyasema hayo jana katika kikao cha Halmashauri hiyo kilichojadili bajeti hiyo jana ambapo amefafanua kuwa mambo hayo matatu ni vipaumbele muhimu kwa halmashauri hiyo.Amesema kuwa fedha hizo zitasaidia kuboresha maabara,mabweni pamoja na kujenga vituo vya afya karibu.
Lumato amesema kuwa upatikanaji wa fedha hizo utasaidia ujenzi wa barabara ya Redio Habari Maalumu,Ngaramtoni,Seliani na Sambasha ambazo pia ni ahadi za Raisi Jakaya Mrisho kikwete.
Naye Mbunge wa Arumeru Magharibi Goodluck Ole Medeye amesema kuwa ni vyema halmashauri ikajikita zaidi kuboresha shule za msingi na sekondari ikiwemo shule ya Sekondari Sokon 2 ambayo inakabiliwana uhaba wa matundu ya choo.
Medeye amewataka wananchi na madiwani kuwa wavumilivu baada ya mashimo ya nguzo kuchimbwa kwenye maeneo yao bila kuwekewa umeme kwanimradi wa umeme vijijini (REA) bado uko kwenye utekelezaji hadi utakapofikia kikomo juni 30 mwaka huu.
“Nawaomba madiwani na wananchi muwe wavumilivu badonafuatilia juu ya mradi wa REA bado wanaendelea na utekelezaji kwasasa kasi yaoinaenda kadiri wanavyopata fedha serikalini” Alisema Medeye
Diwani wa Kata ya Mwandeti Boniface Tarakwa amesemakuwa bajeti hiyo ilenge kukarabati barabara ambazo hazipitiki hasa kipindi cha mvua ili kuboresha miundombinu .
Filed under: HABARI
Jamii imetakiwa kushiriki katika kutatua tatizo la watoto wa mitaani linalozidi kuongezeka kila kukicha badala ya kukaa kimya na kuyaachia mashirika binafsi pamoja na serikali hali inayosababisha tatizo hilo kukua badala ya kupungua.
Hayo yamebainishwa na Meneja Uhusiano wa shirika lisilokuwa la kiserikali la The Foundation of Tommorrow Anton Asukile amesema kuwa jamii imekuwa na mtizamo hasi juu ya watoto wa mitaani na kuwanyooshea vidole huku wakiwatelekeza bila kuchukua hatua jambo ambalo linasababisha tatizo hilo kukosa ukomo .
Anton ameeleza kuwa endapo tatizo la watoto wa mitaani halitatatuliwa linaweza kuwa tatizo kubwa kwa jamii pale ambapo watageuka na kuwa wahalifu,watumiaji wa madawa ya kulevya na majambazi jamii haitasalimika hivyo ni vyema wakavalia njuga suala hilo.
“Mfululizo wa matukio ya uhalifu unaposikia habari za panya road ni hawa hawa watoto wa mitaani wanaungana na kufanya ujambazi na ukatili,jamii isifumbie macho suala hili na kuona kuwa hawahusiki kwani madhara yake yatawakumba na kuwaathiri” Alisema Anton
Amezitaka familia kujenga uchumi imara utakaozisaidia familia zao kupata mahitaji hata inapotokea mzazi mmoja amefariki aliyebakia aweze kuhudumia familia watoto wasisambaratike mitaani kwa kukosa mahitaji muhimu.
Aton amezishauri familia kutatua changamotozinazowakabili pamoja na migogoro inayowakabili ili kuepuka migongano inayopelekea wazazi kutengana na kuwaacha watoto bila msaada hali inayowapelekea kutimikia mitaani.
“Tatizo la watoto wa mitaani ni tatizo la jamii nzima lisipotatuliwa vyema linaweza kugeuka na kuwa janga la taifa hata sasa dalili zimeanza kujitokeza” Alisema Anton
Mratibu wa kituo cha jimolojia Tanzania Bw.Musa Shanyangi akiongea na waandishi wa habari hivikaribuni kuhusu namna kituo hicho kinavyotoa mafunzo ya ukataji madini ya vito
Mwalimu msaidizi wa chuo hicho Bw.Jamal Dallos akiwa anaendelea na shughuli ya ukataji madini
Lilian Petro akikata madini kwaajili ya kutengeneza pete,mkufu ,jiwe hilo ni aina ya Quartz shape Oval
Grace Charles akiendelea na ukataji wa madini
Kulia ni Gladness John pamoja na Loveness Marteen wakiwa wanaendelea na shughuli ya ukataji
Magret Joseph akiwa anaangalia kwa makini namna alivyokuwa akikata jiwe kwa kutumia mashine maalum
Loveness Marteen anachukua fursa hiyo kuwataka wanawake wengine kujitokeza katika fani hiyo ya ukataji madini kwa kuwa hata wanawake wanaweza kufanya shughuli hizo kama wanaume
Aina mbalimbali ya madini kabla ya kukatwa
Baada ya kukatwa na mashine muonekano huwa hivi
Wanafunzi wakiwa darasani wakiwa wanaendelea na shughuli ya ukataji madini
Sekta ya madini nchini bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa walimu na wataalamu wa kufundisha ukataji wa vito vya madini hali inayosababisha kuuzwa kwa madini ghafi nje ya nchi na kupelekea kuuzwa kwa bei ya chini na pesa nyingi kwenda nje
Hayo yameelezwa leo na mratibu wa kituo cha jimolojia Tanzania Bw.Musa Shanyangi wakati akiongea na waandishi wa habari katika kituo hicho kina kinachotoa mafunzo ya ukataji madini ya vito wakati wa mahojiano maalum na waandishi wahabari chuoni hapo ambapo wameanza kutoa mafunzo ngazi ya cheti kwa wahitimu 15 wakike ambapo chuo kipo katika halmashauri ya manispaa ya jiji la arusha.
Alieleza kuwa hivi sasa madini ghafi yanauzwa sana nje ya nchi kwa bei ya chini lakini kama wangeweza kuuza madini hayo yakiwa yameongezwa thaman na kuuzwa kwa bei ghali na kuwezesha fedha za kigen kubaki nchini na kuongeza pato la taifa .
Bw,Shanyangi aliongeza kuwa hivi sasa wameanza kuwafundisha kozi ya miezi 6 kwa wanafunzi 15 wakike ambapo wanafadhiliwa na Arusha women foundation fund iliyoko mjini ikiwa na lengo la kuwasaidia mabinti ili kuweza kusaidia sekta ya madini na kuweza kukabiliana na uhaba wa wataalamu wa ukataji madini nchini.
Hata hivyo kituo hicho kinatarajia kuongeza wanafunzi mpaka kufikia 60 ili kuweza kuongeza ufanisi na kuweza kuboresha sekta hiyo ya madini ili kuweza kuongeza wataalamu ,pia wanamkakati wa kuweza kusomesha walimu wazawa ili kuweza kukidhi nakuwa na walimu na kupunguza gharama za kuchukua mwalimu kutoka nje yanchi ambapo hivi sasa wamemuajiri raia kutoka Sri lanka hali ambayo wanatumia gharama kubwa kumlipa mtaalamu huyo toka nje ya nchi.
BwShanyangi aliwataka wadaumbalimbali nchini pamoja na wawekezaji wawekeze katikak kufundisha wataalamu wazawa ili kuweza kukidhi mahitaji ya wakataji na wataalamu nchini.
Kituo hicho kimegharimu zaidi ya shilingi billion 1.2na mashine mbalimbali za kituoni hapo zimegharimu zaidi ya milioni 450 za ukataji na kusafisha madini hayo
Kwa upande wake mwanafunzi katika chuo hicho Bi.Joice Patrick alisema kuwa kupitia mafunzo hayo ya ukataji wa madini na ung’arishaji itawasaidia katika swala zima la ajira huku akiwataka wanawake kuchangamkia fursa hiyo
“Ni fursa sasa kwa wanawake kujitokeza katika kazi hii na waione kama kazi zingine na si kuwaachia wanaume tu “alisema Joice
![]() |
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassari akitia saini katika kitabu cha wageni katika ofisi ya kata ya Seela Sing’isi alipotembelea katika kijiji hicho cha Sing’isi. |
![]() |
Wananchi wa vijiji vya Sing’isi na Malala wakitizama sehemu ya eneo la Shamba la Madiira lililotolewa kwa wananchi wa vijiji hivyo. |
![]() |
Wananchi wakiwa katika Shamba la Madiira kutizama mipaka ya eneo ambalo limetolewa kwao. |
![]() |
Sehemu ya Shamba la Madiira. |
![]() |
Mbunge Nassari akiwaongoza wananchi wa vijiji vya Sing’isi na Madiira wakitembelea shamaba la Madiira kutizama mipaka ya eneo la Hekari 92 lililotolewa kwao. |
![]() |
Wananchi wakiwa katika kikao cha pamoja. |
Moja ya matrekta waliokabidhiwa wakulima ,Alhaji Omari Kariati ameshatoa matrekta 100 mpaka leo tarehe 5 februari 2015.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba (kushoto) akimsimika kwa kumvalisha joho la ulezi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, mkoani Lindi, Mathias Chikawe, kuwa mlezi wa UWT katika wilaya yake ya Nachingwea. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba (kushoto) akimsimika kwa kumkabidhi fimbo ya ulezi baada ya kumvalisha joho, kofia na skafu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, mkoani Lindi, Mathias Chikawe, kuwa mlezi wa UWT katika wilaya yake ya Nachingwea. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo. Wapili kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo, Regina Chonjo, na wapili kushoto ni mwanachama wa UWT wilayani humo, ambaye pia ni Mke wa Waziri Chikawe, Profesa Amandina Lyamba.
Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo (kushoto), Mke wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe, Profesa Amandina Lyamba (kulia) wakilisakata rumba na wanachama wenzao wa Umoja wa Wanawake (UWT) wilayani humo baada ya Mbunge wao kusimikwa rasmi na Mwenyekiti wa UWT Taifa, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, kuwa mlezi wa UWT katika wilaya yake ya Nachingwea. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo.
Mlezi wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Nachingwea, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto), akipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa UWT wilayani humo baada ya Waziri huyo kusimikwa na rasmi na Mwenyekiti UWT Taifa, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba (kushoto kwa Chikawe), kuwa mlezi wa UWT wilayani humo. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba akizungumza kwa furaha wakati akitoa hotuba yake kwa wananchama wa UWT Wilaya ya Nachingwea baada ya kumsimika Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto) kuwa mlezi wa UWT wilayani humo. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo. Katika hotuba yake hiyo, Waziri Simba alimuomba Waziri Chikawe aendelee kuisaidia UWT wilayani humo kama alivyokuwa anafanya awali. Kulia ni Mwenyekiti wa UWT, Mkoa wa Lindi, Faudhia Chiwangu.
Mlezi wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Nachingwea, ambaye pia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akiwashukuru wanachama wa UWT wilayani humo kwa kumchagua kuwa mlezi wa umoja wao katika sherehe ya kusimikwa kwake iliyofanyika mjini Nachingwea leo. Katika hotuba yake, Waziri Chikawe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, aliwaomba wanachama hao kuwa na ushirikiano kwa kuijenga CCM, pamoja na kuhakikisha wanawahamasisha wananchi jimboni humo kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ili kujiandaa kwa kuipigia kura Katiba iliyopendekezwa pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao. Kulia ni Mwenyekiti UWT Taifa, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba ambaye alimsimika mlezi huyo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Regina Chonjo.
Mlezi wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Nachingwea, ambaye pia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia), Mwenyekiti UWT Taifa, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba (katikati) na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Nachingwea, Ng’ondomole Modesta Makota wakiwaaga mamia ya wanachama wa UWT wilayani humo (hawapo pichani) wakati walipokuwa wanatoka ukumbini. Waziri Chikawe alisimikwa na Waziri Simba ili awe mlezi wa umoja huo na kuhakikisha kuwa UWT wilayani humo inazidi kusonga mbele. Sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wanachama wa UWT, ilifanyika katika Ukumbi wa NR mjini Nachingwea leo.
Katika picha ni Noel Olevaroya akihutubia Maelfu ya wananchi katika moja ya harakati zake katika mkutano wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa vijana na mjumbe Wilaya ya Arusha kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)Noel Olevaroya (37) ametangaza rasmi kupeperusha bendera ya chama hicho kwa kuwania nafasi ya ubunge katika jimbo la Arusha mjini
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha Noel Olevaroya alisema kuwa nia yake ya kugombea nafasi ya ubunge katika jimbo la Arusha ni msukumumo kutoka kwa Mungu baada ya kumaliza nafasi yake ya uwenyekiti wa vijana na mjumbe wilaya ya Arusha mwaka 2014
Alieleza kuwa msukumo huo ulikuwa ukimsumbua sana na ndipo aliamua kutii sauti ya Mungu kwa kutangaza kuwania nafasi hiyo ya kugombea kiti cha ubunge katika jimbo la Arusha mjini ambapo kwasasa jimbo hilo lipo mikononi mwa Godbless Lema
Aidha alisema kuwa Mbunge anafursa nzuri sana ya kusaidia wananchi hata kwa kupitia mfuko wa jimbo,mshahara hali ambayo itasaidia kuwainua wananchi na kupunguza umaskini
Alitoa wito kwa vijana wa Arusha kusikiliza sauti ya Mungu kwa kuwachagua viongozi bora wenye hofu ya Mungu kwa maslahi ya Nchi yetu
Filed under: HABARI
![]() |
Mwenyekiti wa Chadema Freman Mbowe akiwa anasoma utuba wakati wa ufunguzi wa mkutano wa viongozi wa chama hicho wa kanda ya kaskazini unaofanyika leo katika hotel ya new Arusha jijini hapa |